Mabingwa wa kihistoria wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga SC wameendelea kuwa moto baada ya leo kuichapa Mbeya City mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Magoli ya Yanga yamefungwa na mshambuliaji Heritier Makambo dakika ya 17 na 41 huku bao la Mbeya City likifungwa na Iddy Selemani ‘Naldo’ dakika ya 24.