Afisa wa Polisi kutoka Arusha anaehudumu Umoja wa Mataifa nchini Congo, Ally Babu amewahasa Watanzania wanaopata nafasi kwenda nje ya nchi kukumbuka kutangaza vivutio vya Utalii vyaTanzania pamoja na kuwaelezea fursa za uwekezaji.
Babu ambaye pia ni Mwanasheria ameyasema hayo wakati wa tafrija ya chakula cha jioni kwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa nchini Congo.